contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, September 9, 2011

OBAMA kuwekeza katika elimu tena, KIKWETE......??

raisi Barrack Obama
 Raisi wa marekani Barrack Hussein Obama amewasilisha mpango unaoazimia kufufua uchumi na kutoa nafasi mpya za ajira utakaogharimu dola za kimarekani billion 450
Katika hotuba yake iliyokua ikingojewa kwa hamu, Obama ameliambia bunge la marekani, lengo ni kufufua uchumi wa marekani uliozorota, kutoa nafasi mpya za ajira na kuwapa vijana matumaini
Kiini cha mpango huo ni kupunguza gharama za ruzuku ya serikali kwa wale wasiojiweza na kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu na miundo mbinu, pia ameongeza kuwa atabadilisha mfumo wa kodi uwe ni wa haki kwa kila mmoja
rais Jakaya Kikwete
Raisi wetu kikwete tungependa uige mifano kama hii, kodi  sawa kwa wwote, rasilimali ziwasaidie wananchi wa hali zote na sio wanaojiweza tu na kikubwa zaidi ni kuwekeza katika elimu, walimu ni wachache nao pia kila kukicha wanalalamika mishahara haiwatoshelezi mahitaji yao, wanafunzi wa vyuo vikuu wanagoma kila kukicha wakidai  mikopo, shule  za kata nyingi lakini vitabu hakuna, wakati huo huo mshahara wa mbunge kwa mwezi ni sawa na mshahara  wa mwalimu wa kawaida kwa mwaka mzima

No comments:

Post a Comment