contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, September 9, 2011

NIGER KUMSHUGHULIKIA GADDAFI

Col. Muammar Gaddafi
 Serikali ya Niger imesema kuwa itaamua jinsi ya kushughulika na kanali Muamar Gaddafi iwapo ataingia nchini humo kuomba hifadhi ya kisiasa
Kanali Muamar Gaddafi
Ripoti kutoka eneo hilo zimesema maofisa wa  vyeo vya juu katika serikali iliyotimuliwa wamewasili nchini Niger na kuna habari kuwa huenda Gaddafi akajiunga nao. Baraza la mpito la Libya limetoa wito kwa serikali ya Niger isimpe hifadhi kanali Gaddafi
Kanali Gaddafi na walinzi wake wa kike
 wakati huo huo Kanali Gaddafi amepuuza madai kwamba ametorokea nchi jirani ya Niger na kuyataja madai hayo kama uongo  na vita vya kiakili. Matamshi ya Gaddafi yamepeperushwa na kituo kimoja cha TV nchini Sirya kilichodai kuwa Kanali Gaddafi bado yupo nchini Libya. Gaddafi ameapa  kuwashinda wapiganaji wa upinzani wanaoungwa mkono na majeshi ya NATO. Huu ni ujumbe  wake wa kwanza katika kipindi kirefu
Walinzi wa Kanali Gaddafi
.
Baraza la kitaifa la mpito la Libya limetoa wito kwa Niger kutompa hifadhi Kanali Gaddafi. Serikali ya  Niger imesema kwamba itaamua yenyewe jinsi itakavyomshughulikia Gaddafi ikiwa ataingia nchini humo

No comments:

Post a Comment