Sept 7, 2011 serikali ya Marekani kupitia balozi wake nchini imewasilisha msaada wa (1,132,000,000.00) shilingi za kitanzania, karibia bilioni moja na robo kusaidia utunzaji wa hifadhi za kumbukumbu za Kilwa
ufukwe wa bahari, Kilwa
Hifadhi hizo ambazo zimekuwepo tangu karne ya 19 zinatakiwa kutunzwa ili ziendelee kuwa kivutio kizuri cha utalii nchini na kuingizia taifa kipato zaidi. Msaada huo uliopita chini ya US Department of State's Ambassadors Fund for Cultural Preservation (AFCP) umetolewa kwa lengo la kusaidia utunzaji wa hifadhi za mambo ya kale Africa Mashariki na pia kuwawezesha wakazi wa maeneo hayo kunufaika na hifadhi hizo
No comments:
Post a Comment