Kwa takribani miaka minne sasa, kumekuwepo na mvutano kati ya Taasisi ya ustawi wa jamii (ISW) na Baraza la taifa la Elimu ya juu na ufundi (NACTE), kuhusu masuala ya taaluma katika taasisi hiyo. Mvutano huo uliwasukuma baadhi ya wahadhiri katika taasisi hiyo kushinikiza menejimenti yao kutekeleza mapendekezo ya baraza hilo kuboresha taaluma, lakini kilichowakuta wahadhiri hao, licha ya juhudi zote zilizofanywa na vyombo mbalimbali kujaribu kurekebisha mambo katika taasisi hiyo, bodi ya chuo iliridhia kuwafukuza kazi wahadhiri 21 mnamo agosti 21 mwaka huu, ambao kosa lao pekee kubwa ni kutaka taaluma iboreshwe katika chuo hicho
Wahadhiri hao wamefukuzwa kwa madai kwamba waliendesha mgomo usio halali na kukaidi maagizo ya mamlaka za juu
Mambo bado si shwari katika taasisi hiyo, mpaka sasa hakuna maboresho yoyote ya maana ya kitaaluma yaliyofanyika, bali kinachoendelea pale ni migogoro ambayo hatma yake ni kuzalisha wahitimu walio chini ya kiwango wasioweza kushindana vyema katika soko gumu la ajira nchini
Ukweli ni kwamba, kiini cha migogoro ni taasisi kuendelea kupuuza maagizo ya NACTE. kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kwamba barua za NACTE zenye kumbukumbu NACTE/ DA/ 31/655/Vol 1./92 ya june 19/ 19/ 2010; zinaonyesha taasisi ya ustawi wa jamii ilipewa maagizo ya kufanya maboresho ili kukidhi matakwa ya ithibati yanayokubalika NACTE
Kwa mshangao, menejimenti iliamua kukaidi maagizo hayo ya NACTE. Na hili ndilo pia lililosababisha wahadhiri watatu waandamizi wa chuo hicho -Dk Mihanja, Dk Matiku na Dk Kitojo kujiuzulu kazi mwaka 2007.
Ukaidi huo ulisababisha taasisi kuzuiliwa kujihusisha na udahili wa programu za ngazi ya cheti, stashahada na shahada (certificate, diploma, degree programs) ilipofika April 2011, kwa kuwa ilishindwa kukidhi matakwa ya ithibati ya kwanza iliyoidhinishwa na NACTE kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2006-2011
Kwa barua hizo taasisi ilipewa muda mpya wa kuandaa mitaala na kurekebisha mfumo wa utawala hadi ifikapo septemba 2011 ili warudishiwe haki ya kuendesha program hizo, mpaka wiki mbili zilizopita hilo lilikuwa halijatendeka
Kwa ufupi, si kweli kwamba tatizo la taasisi hiyo lilikua ni hao wadhahiri waliofukuzwa kazi kama inavyodaiwa, wao walikuwa wakipigania taasisi hiyo kutii maagizo yaliyotolewa na NACTE. Si kweli kwamba waliachishwa kazi kwa kufanya mgomo usio halali, na si kweli kwamba kwa kuwafukuza kazi, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo itaboresheka, ni mpaka hapo hilo litakapozingatiwa, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo haiwezi kuwa shwari, kwa sababu wahitimu wa taasisi hiyo wataendelea kuwa chini ya viwango na ajira zitaendelea kuwakimbia
menejimenti ya taasisi hiyo imekiuka haki za msingi za wafanyakazi walioachishwa kazi bila kufuata kanuni za ajira za taasisi ya ustawi wa jamii (staff regulation) na sheria ya kazi Na.6 ya mwaka 2004, na kwa mujibu wa katiba ya nchi, pia imewadhalilisha wadhahiri hao walioachishwa kazi wakipigania maslahi ya taasisi, maslahi ya wanafunzi na maslahi ya umma mzima wa Tanzania
Wednesday, September 21, 2011
Monday, September 19, 2011
SOKO LA SIDO MWANJELWA MBEYA LATEKETEA KWA MOTO
Mbunge wa Mbeya mjini, Mh Joseph Mbilinyi aka Sugu akiwa ametembelea soko la SIDO mwanjelwa jijini Mbeya likiwa linateketea kwa moto |
Mabanda ya soko yakiteketea, kikosi cha kuzima moto cha jiji hili kilifika eneo la tukio kuzima moto na kuokoa watu na mali zao kikiwa na gari bovu na pia likiwa halina maji ya kuzimia moto huu |
AJALI YA MELI ZANZIBAR
Muonekano wa nje wa meli ya MV Spice Islander kabla ya kupata ajali, meli hii inasemekana ilibeba abiria zaidi ya 1500, idadi ambayo ni zaidi ya mara mbili ya idadi ya abiria inayopaswa kubeba |
Baadhi ya miili ya abiria iliyopatikana katika ajali hiyo, mamia ya watu wamepoteza uhai katika ajali hii |
Baadhi ya wahanga wa ajali hii waliofanikiwa kuokolewa |
Makaburi yaliyochimbwa Zanzibar kwa ajili ya kuwazika marehemu wa ajali ya meli |
Askari na raia wakijitahidi kuokoa abiria waliosalimika katika ajali hiyo, kikosi cha jeshi la polisi wanamaji KMKM na JKU bado vinaendelea na utafutaji wa miili ya abiria wengine wa ajali hiyo |
muonekano wa meli ya MV spice ikiwa inaendelea kuzama ndani ya maji |
Baadhi ya miili ya watoto wadogo waliopoteza maisha katika ajali ya meli |
Friday, September 9, 2011
MAMILIONI KUMWAGIKA KISIWANI KILWA
shehemu ya mabaki ya kilwa |
ufukwe wa bahari, Kilwa |
sehemu ya mabaki ya Kilwa |
NIGER KUMSHUGHULIKIA GADDAFI
Col. Muammar Gaddafi |
Kanali Muamar Gaddafi |
Kanali Gaddafi na walinzi wake wa kike |
Walinzi wa Kanali Gaddafi |
Baraza la kitaifa la mpito la Libya limetoa wito kwa Niger kutompa hifadhi Kanali Gaddafi. Serikali ya Niger imesema kwamba itaamua yenyewe jinsi itakavyomshughulikia Gaddafi ikiwa ataingia nchini humo
OBAMA kuwekeza katika elimu tena, KIKWETE......??
raisi Barrack Obama |
Katika hotuba yake iliyokua ikingojewa kwa hamu, Obama ameliambia bunge la marekani, lengo ni kufufua uchumi wa marekani uliozorota, kutoa nafasi mpya za ajira na kuwapa vijana matumaini
Kiini cha mpango huo ni kupunguza gharama za ruzuku ya serikali kwa wale wasiojiweza na kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu na miundo mbinu, pia ameongeza kuwa atabadilisha mfumo wa kodi uwe ni wa haki kwa kila mmoja
rais Jakaya Kikwete |
WANAFUNZI WAVAMIA OFISI ZA TCU
wanafunzi wakiwa katika maandamano |
wanafunzi wakiwa katika maandamano |
BODI YA MIKOPO KUCHUNGUZA TENA UTOAJI WA MKOPO KWA WALIOKOSA
bodi ya mikopo elimu ya juu |
wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi imetoa muda wa wiki mbili kwa bodi ya mikopo kupitia upya majina ya wanafunzi waliokosa mikopo lakini wakiwa na vigezo vyote vya kupata mikopo
imeshangaza kuona ni idadi ndogo tu ya wanafunzi walioomba mikopo kwa mwaka wa masomo 2011\12 wamefanikiwa kupata mikopo hiyo ikiacha idadi kubwa wakiwa wamekosa. HELSB imekubali kufanya uhakiki huo na bila shaka baada ya wiki mbili tutajua majibu kamili
baadhi ya viongozi HELSB |
Monday, September 5, 2011
Hatma ya wanafunzi wa INTENATIONAL RELATIONS chuo kikuu cha dodoma
Kutokana na migomo ya hapa na pale iliyofanywa na wanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma, ililazimu chuo hicho kufungwa na wanafunzi wote wakarudishwa nyumbani wakiambiwa kusubiri hadi watakapoitwa tena chuoni hapo, wanafunzi wa kozi nyingine zote wameitwa kurudi chuo na kuendelea na masomo isipokua wanafunzi wanaosomea INTERNATIONAL RELATIONS kwa madai kuwa wao ndio walikua wachochezi wakubwa wa migomo, swali lagu ni kutaka kujua nini hasa hatma ya wanafunzi hawa??
Subscribe to:
Posts (Atom)