contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, November 24, 2011

MIGOMO SIO ISHU

Kwa mtazamo wangu kiukweli mimi sioni faida ya migomo no matter tunapigania kitu gani, hii ni kutokana na mambo yaliotokea hapa juzikati, baaadhi ya wanafunzi wameumizwa kwa kupigwa na askari, wengine tumeumizwa na mabomu ya machozi, hii sio mara ya kwanza kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kugoma na kuandamana, kama kweli migomo ingekua inasaidia, haya matatizo yasingekua yanajirudia, tutaendelea kupigwa mabomu ya machozi na mwisho wa siku tutakuja kupigwa hata na risasi za moto na matatizo yataendelea kujirudia kama kawa, me nashauri tungejaribu kutafuta njia nyingine ya kuwafanya hawa viumbe watuelewe, kuna wanafunzi wa mwaka wa kwanza pia wameandamana, nyie hamjafikisha hata semista moja hapa chuo mmeshaanza kujiingiza matatizoni, mkiumizwa au kufukuzwa chuo mtawaelezea habari gani wazazi wenu ambao wanajinyima ili nyie mpate elimu, acheni kufata mkumbo wadogo zangu, someni, hicho ndicho kilichowaleta UDSM.

Friday, November 4, 2011

CHUO CHA MAENDELEO NA USIMAMIZI WA MAJI (WDMI)

          Jina chuo cha maendeleo na usimamizi wa maji linaweza kuwa geni masikioni mwa watu, lakini chuo hichi ni moja kati ya vyuo vikongwe hapa nchini, kilianzishwa mwaka 1974 kikijulikana kama RWEGALULILA WATER RESOURCE INSTITUTE, dhumuni kubwa ikiwa ni wataalam katika fani mbalimbali zinazohusu MAJI.
         Kubadilika kwa jina na kuwa WATER DEVELOPMENT AND MANADEMENT INSTITUTE, ilifanyika mwaka 2008, baada ya chuo kupewa hadhi ya kuwa wakala wa serikali yaani Agency, mpaka sasa chuo kinatoa kozi tano katika ngazi ya Diploma, WATER SUPPLY AND SANITATION ENGINEERING, HYDOGEOLOGY AND WATER WELL DRILLING. HYDROLOGY AND METROLOGY, WATER LABORATORY TECHNOLOGY na IRRIGATION ENGINEERING. Mipango ya degree kuanza imekamilika na muda wowote WATER RESOURCE AND IRRIGATION ENGINEERING  itaanza, sasa kazi kwenu nyie wenye hamu ya kufanya kazi kwenye sekta ya maji, mnakaribishwa sana.