contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, September 19, 2011

AJALI YA MELI ZANZIBAR

abiria wa meli ya MV Spice Islander ilyopata ajali usiku wa kuamkia septemba 10,2011 ikiwa inaelekea Pemba  kutokea Dar es salaam wakijitahidi kuokoa uhai kwao kwa kutumia magodoro yaliyokuwamo katika meli hiyo

Muonekano wa nje wa meli ya MV Spice Islander kabla ya kupata ajali, meli hii inasemekana ilibeba abiria zaidi ya 1500, idadi ambayo ni zaidi  ya mara mbili ya idadi ya abiria inayopaswa kubeba

Baadhi ya miili ya abiria iliyopatikana katika ajali hiyo, mamia ya watu wamepoteza uhai katika ajali hii

Baadhi ya wahanga wa ajali hii waliofanikiwa kuokolewa

Makaburi yaliyochimbwa Zanzibar kwa ajili ya kuwazika marehemu wa ajali ya meli

Meli ya MV Spice ikiwa imepinduka maeneo ya Nungwi, meli hii iliondoka bandari Zanzibar kuelekea jioni ya tarehe 9 septemba, ilianza kuzama mida ya saa 3 usiku na hatimaye kupinduka  na kuzama kabisa, meli hii ilielemewa na mizigo na idadi kubwa ya abiria

Askari na raia wakijitahidi kuokoa abiria waliosalimika katika ajali hiyo, kikosi cha jeshi la polisi wanamaji KMKM na JKU bado vinaendelea na utafutaji wa miili ya abiria wengine wa ajali hiyo

muonekano  wa meli ya MV spice ikiwa inaendelea kuzama ndani ya maji

Baadhi ya miili ya watoto wadogo waliopoteza maisha katika ajali ya meli

Ndugu na jamaa wakiwaombea watu waliopoteza maisha katika ajali ya meli Zanzibar. hii ni meli ya pili kuzama ikielekea Pemba, nyingine ni MV Fatahi iliyozama mwaka jana ikiwa bandari zanzibar kuelekea Pemba

No comments:

Post a Comment