contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, August 10, 2011

YANGA FC, HII NI DHARAU AU TUWAELEWEJE???

 TFF ilitishia kuchukua hatua kali kwa club ya Yanga endapo club iyo ingegoma kuwaruhusu wachezaji wao nane kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars ambayo leo jumatano, siku ya kalenda ya FIFA kwa mechi za kimataifa, inatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki na sudan huko jijini Khartoum. Yanga imejitetea kuwa walipata mwaliko huo kabla kabla ya wachezaji hao kuitwa timu ya taifa hivyo wana haki ya kuwatumia licha ya ukweli kwamba TFF ina haki zaidi kwani siku hii inatambuliwa na FIFA kwa kuwa ipo kwaenye kalenda ya mechi za timu za taifa na club zinawajibika kuwatoa wachezaji wote wanaoitwa. 
 Sasa Yanga kwa kitendo mlichokifanya kuwazuia wachezaji wenu wasishiriki kuichezea timu yetu ya taifa mnataka watanzania tuwaeleweje, mbona mnakosa uzalendo kiasi hiki??
Kocha wa timu ya taifa, Paulsen imebidi aokote wachezaji ambao hawakua katika list yake, sisemi kama hawana kiwango cha kutosha kuichezea timu yetu ya taifa ila kuna mambo mengi watakua wameyakosa kama kuzoeana uwanjani na mbinu ambazo wachezaji wa siku zote hufundishwa na kocha huyo, hivi timu yetu isipofanya vizuri tumlaumu Paulsen kama tulivofanya kwa Maximo au?
YANGA FC, HII NI DHARAU!!

No comments:

Post a Comment