Thursday, November 24, 2011
MIGOMO SIO ISHU
Kwa mtazamo wangu kiukweli mimi sioni faida ya migomo no matter tunapigania kitu gani, hii ni kutokana na mambo yaliotokea hapa juzikati, baaadhi ya wanafunzi wameumizwa kwa kupigwa na askari, wengine tumeumizwa na mabomu ya machozi, hii sio mara ya kwanza kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kugoma na kuandamana, kama kweli migomo ingekua inasaidia, haya matatizo yasingekua yanajirudia, tutaendelea kupigwa mabomu ya machozi na mwisho wa siku tutakuja kupigwa hata na risasi za moto na matatizo yataendelea kujirudia kama kawa, me nashauri tungejaribu kutafuta njia nyingine ya kuwafanya hawa viumbe watuelewe, kuna wanafunzi wa mwaka wa kwanza pia wameandamana, nyie hamjafikisha hata semista moja hapa chuo mmeshaanza kujiingiza matatizoni, mkiumizwa au kufukuzwa chuo mtawaelezea habari gani wazazi wenu ambao wanajinyima ili nyie mpate elimu, acheni kufata mkumbo wadogo zangu, someni, hicho ndicho kilichowaleta UDSM.
Friday, November 4, 2011
CHUO CHA MAENDELEO NA USIMAMIZI WA MAJI (WDMI)
Jina chuo cha maendeleo na usimamizi wa maji linaweza kuwa geni masikioni mwa watu, lakini chuo hichi ni moja kati ya vyuo vikongwe hapa nchini, kilianzishwa mwaka 1974 kikijulikana kama RWEGALULILA WATER RESOURCE INSTITUTE, dhumuni kubwa ikiwa ni wataalam katika fani mbalimbali zinazohusu MAJI.
Kubadilika kwa jina na kuwa WATER DEVELOPMENT AND MANADEMENT INSTITUTE, ilifanyika mwaka 2008, baada ya chuo kupewa hadhi ya kuwa wakala wa serikali yaani Agency, mpaka sasa chuo kinatoa kozi tano katika ngazi ya Diploma, WATER SUPPLY AND SANITATION ENGINEERING, HYDOGEOLOGY AND WATER WELL DRILLING. HYDROLOGY AND METROLOGY, WATER LABORATORY TECHNOLOGY na IRRIGATION ENGINEERING. Mipango ya degree kuanza imekamilika na muda wowote WATER RESOURCE AND IRRIGATION ENGINEERING itaanza, sasa kazi kwenu nyie wenye hamu ya kufanya kazi kwenye sekta ya maji, mnakaribishwa sana.
Kubadilika kwa jina na kuwa WATER DEVELOPMENT AND MANADEMENT INSTITUTE, ilifanyika mwaka 2008, baada ya chuo kupewa hadhi ya kuwa wakala wa serikali yaani Agency, mpaka sasa chuo kinatoa kozi tano katika ngazi ya Diploma, WATER SUPPLY AND SANITATION ENGINEERING, HYDOGEOLOGY AND WATER WELL DRILLING. HYDROLOGY AND METROLOGY, WATER LABORATORY TECHNOLOGY na IRRIGATION ENGINEERING. Mipango ya degree kuanza imekamilika na muda wowote WATER RESOURCE AND IRRIGATION ENGINEERING itaanza, sasa kazi kwenu nyie wenye hamu ya kufanya kazi kwenye sekta ya maji, mnakaribishwa sana.
Monday, October 24, 2011
WANACHUO SJMC KUANDAMANA BODI YA MIKOPO LEO
Licha ya wanafunzi kupiga kelele kibao na migomo ya hapa na pale kuielekea bodi ya mikopo ya elimu ya juu Tanzania, bodi hiyo inaonyesha live kutozingatia kwa kuendelea kuchelewesha mikopo ya wanafunzi. Hii inatokana na wanafunzi wa mwaka wa tatu katika chuo kikuu cha Dar es Salaam kitengo cha uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma (sjmc) kutopata mkopo wao hadi leo, Wanafunzi wa chuo hicho sasa hivi wameamua kwenda bodi ya mikopo ili wakapate kujua ni ishu gani inaendelea na kwanini haya matatizo hayaishi, ni uzembe tu wa wafanyakazi au inakuaje, tunakoelekea kama tatizo hili litaendelea itakua balaa, Bodi kaeni chonjo mmeshatuchosha
Wednesday, September 21, 2011
UKWELI KUHUSU MIGOGORO YA CHUO CHA USTAWI WA JAMII
Kwa takribani miaka minne sasa, kumekuwepo na mvutano kati ya Taasisi ya ustawi wa jamii (ISW) na Baraza la taifa la Elimu ya juu na ufundi (NACTE), kuhusu masuala ya taaluma katika taasisi hiyo. Mvutano huo uliwasukuma baadhi ya wahadhiri katika taasisi hiyo kushinikiza menejimenti yao kutekeleza mapendekezo ya baraza hilo kuboresha taaluma, lakini kilichowakuta wahadhiri hao, licha ya juhudi zote zilizofanywa na vyombo mbalimbali kujaribu kurekebisha mambo katika taasisi hiyo, bodi ya chuo iliridhia kuwafukuza kazi wahadhiri 21 mnamo agosti 21 mwaka huu, ambao kosa lao pekee kubwa ni kutaka taaluma iboreshwe katika chuo hicho
Wahadhiri hao wamefukuzwa kwa madai kwamba waliendesha mgomo usio halali na kukaidi maagizo ya mamlaka za juu
Mambo bado si shwari katika taasisi hiyo, mpaka sasa hakuna maboresho yoyote ya maana ya kitaaluma yaliyofanyika, bali kinachoendelea pale ni migogoro ambayo hatma yake ni kuzalisha wahitimu walio chini ya kiwango wasioweza kushindana vyema katika soko gumu la ajira nchini
Ukweli ni kwamba, kiini cha migogoro ni taasisi kuendelea kupuuza maagizo ya NACTE. kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kwamba barua za NACTE zenye kumbukumbu NACTE/ DA/ 31/655/Vol 1./92 ya june 19/ 19/ 2010; zinaonyesha taasisi ya ustawi wa jamii ilipewa maagizo ya kufanya maboresho ili kukidhi matakwa ya ithibati yanayokubalika NACTE
Kwa mshangao, menejimenti iliamua kukaidi maagizo hayo ya NACTE. Na hili ndilo pia lililosababisha wahadhiri watatu waandamizi wa chuo hicho -Dk Mihanja, Dk Matiku na Dk Kitojo kujiuzulu kazi mwaka 2007.
Ukaidi huo ulisababisha taasisi kuzuiliwa kujihusisha na udahili wa programu za ngazi ya cheti, stashahada na shahada (certificate, diploma, degree programs) ilipofika April 2011, kwa kuwa ilishindwa kukidhi matakwa ya ithibati ya kwanza iliyoidhinishwa na NACTE kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2006-2011
Kwa barua hizo taasisi ilipewa muda mpya wa kuandaa mitaala na kurekebisha mfumo wa utawala hadi ifikapo septemba 2011 ili warudishiwe haki ya kuendesha program hizo, mpaka wiki mbili zilizopita hilo lilikuwa halijatendeka
Kwa ufupi, si kweli kwamba tatizo la taasisi hiyo lilikua ni hao wadhahiri waliofukuzwa kazi kama inavyodaiwa, wao walikuwa wakipigania taasisi hiyo kutii maagizo yaliyotolewa na NACTE. Si kweli kwamba waliachishwa kazi kwa kufanya mgomo usio halali, na si kweli kwamba kwa kuwafukuza kazi, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo itaboresheka, ni mpaka hapo hilo litakapozingatiwa, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo haiwezi kuwa shwari, kwa sababu wahitimu wa taasisi hiyo wataendelea kuwa chini ya viwango na ajira zitaendelea kuwakimbia
menejimenti ya taasisi hiyo imekiuka haki za msingi za wafanyakazi walioachishwa kazi bila kufuata kanuni za ajira za taasisi ya ustawi wa jamii (staff regulation) na sheria ya kazi Na.6 ya mwaka 2004, na kwa mujibu wa katiba ya nchi, pia imewadhalilisha wadhahiri hao walioachishwa kazi wakipigania maslahi ya taasisi, maslahi ya wanafunzi na maslahi ya umma mzima wa Tanzania
Wahadhiri hao wamefukuzwa kwa madai kwamba waliendesha mgomo usio halali na kukaidi maagizo ya mamlaka za juu
Mambo bado si shwari katika taasisi hiyo, mpaka sasa hakuna maboresho yoyote ya maana ya kitaaluma yaliyofanyika, bali kinachoendelea pale ni migogoro ambayo hatma yake ni kuzalisha wahitimu walio chini ya kiwango wasioweza kushindana vyema katika soko gumu la ajira nchini
Ukweli ni kwamba, kiini cha migogoro ni taasisi kuendelea kupuuza maagizo ya NACTE. kumbukumbu zilizopo zinaonyesha kwamba barua za NACTE zenye kumbukumbu NACTE/ DA/ 31/655/Vol 1./92 ya june 19/ 19/ 2010; zinaonyesha taasisi ya ustawi wa jamii ilipewa maagizo ya kufanya maboresho ili kukidhi matakwa ya ithibati yanayokubalika NACTE
Kwa mshangao, menejimenti iliamua kukaidi maagizo hayo ya NACTE. Na hili ndilo pia lililosababisha wahadhiri watatu waandamizi wa chuo hicho -Dk Mihanja, Dk Matiku na Dk Kitojo kujiuzulu kazi mwaka 2007.
Ukaidi huo ulisababisha taasisi kuzuiliwa kujihusisha na udahili wa programu za ngazi ya cheti, stashahada na shahada (certificate, diploma, degree programs) ilipofika April 2011, kwa kuwa ilishindwa kukidhi matakwa ya ithibati ya kwanza iliyoidhinishwa na NACTE kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2006-2011
Kwa barua hizo taasisi ilipewa muda mpya wa kuandaa mitaala na kurekebisha mfumo wa utawala hadi ifikapo septemba 2011 ili warudishiwe haki ya kuendesha program hizo, mpaka wiki mbili zilizopita hilo lilikuwa halijatendeka
Kwa ufupi, si kweli kwamba tatizo la taasisi hiyo lilikua ni hao wadhahiri waliofukuzwa kazi kama inavyodaiwa, wao walikuwa wakipigania taasisi hiyo kutii maagizo yaliyotolewa na NACTE. Si kweli kwamba waliachishwa kazi kwa kufanya mgomo usio halali, na si kweli kwamba kwa kuwafukuza kazi, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo itaboresheka, ni mpaka hapo hilo litakapozingatiwa, hali ya kitaaluma ya taasisi hiyo haiwezi kuwa shwari, kwa sababu wahitimu wa taasisi hiyo wataendelea kuwa chini ya viwango na ajira zitaendelea kuwakimbia
menejimenti ya taasisi hiyo imekiuka haki za msingi za wafanyakazi walioachishwa kazi bila kufuata kanuni za ajira za taasisi ya ustawi wa jamii (staff regulation) na sheria ya kazi Na.6 ya mwaka 2004, na kwa mujibu wa katiba ya nchi, pia imewadhalilisha wadhahiri hao walioachishwa kazi wakipigania maslahi ya taasisi, maslahi ya wanafunzi na maslahi ya umma mzima wa Tanzania
Monday, September 19, 2011
SOKO LA SIDO MWANJELWA MBEYA LATEKETEA KWA MOTO
![]() |
| Mbunge wa Mbeya mjini, Mh Joseph Mbilinyi aka Sugu akiwa ametembelea soko la SIDO mwanjelwa jijini Mbeya likiwa linateketea kwa moto |
![]() |
| Mabanda ya soko yakiteketea, kikosi cha kuzima moto cha jiji hili kilifika eneo la tukio kuzima moto na kuokoa watu na mali zao kikiwa na gari bovu na pia likiwa halina maji ya kuzimia moto huu |
AJALI YA MELI ZANZIBAR
![]() |
| Muonekano wa nje wa meli ya MV Spice Islander kabla ya kupata ajali, meli hii inasemekana ilibeba abiria zaidi ya 1500, idadi ambayo ni zaidi ya mara mbili ya idadi ya abiria inayopaswa kubeba |
![]() |
| Baadhi ya miili ya abiria iliyopatikana katika ajali hiyo, mamia ya watu wamepoteza uhai katika ajali hii |
![]() |
| Baadhi ya wahanga wa ajali hii waliofanikiwa kuokolewa |
![]() |
| Makaburi yaliyochimbwa Zanzibar kwa ajili ya kuwazika marehemu wa ajali ya meli |
![]() |
| Askari na raia wakijitahidi kuokoa abiria waliosalimika katika ajali hiyo, kikosi cha jeshi la polisi wanamaji KMKM na JKU bado vinaendelea na utafutaji wa miili ya abiria wengine wa ajali hiyo |
![]() |
| muonekano wa meli ya MV spice ikiwa inaendelea kuzama ndani ya maji |
![]() |
| Baadhi ya miili ya watoto wadogo waliopoteza maisha katika ajali ya meli |
Friday, September 9, 2011
MAMILIONI KUMWAGIKA KISIWANI KILWA
![]() |
| shehemu ya mabaki ya kilwa |
![]() |
| ufukwe wa bahari, Kilwa |
![]() |
| sehemu ya mabaki ya Kilwa |
Subscribe to:
Posts (Atom)















