contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, August 23, 2011

HII NI KWA SJMC STUDENTS...........................

kutakana na sababu siziweza kuzuilika, matokeo ya wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam kitivo cha uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma (SJMC) yamekua ya mwisho kutolewa ukilinganisha na vitivo vingine, lakini tatizo hilo lilishashughulikiwa na sasa wanafunzi wa SJMC wanaweza wakayapata matokeo hayo katika mtandao wa ARIS, go and check what you sow guys, skulliz blog wishes you all the luck in the world, love you all

Monday, August 22, 2011

ARIS ARIS ARIS, MATOKEO YAMETOKA

Matokeo ya wanachuo kikuu cha dar es salaam yametoka katika mtandao wa Aris, wanafunzi wote waliofanya mtihani wanashauriwa kuangalia matokeo yao katika mtandao huo, incase kuna tatizo lolote katika matokeo yako, muone class representative wako as soon as possible.
Ninaamini hakuna atakaekua amefanya vibaya sana, na kwa wale wote waliopata sup, poleni sana, jitahidini sana mkasapue izo sup zenu coz hatutaki kuwapoteza chuoni, skulliz blog wishes you all the best

Wednesday, August 10, 2011

YANGA FC, HII NI DHARAU AU TUWAELEWEJE???

 TFF ilitishia kuchukua hatua kali kwa club ya Yanga endapo club iyo ingegoma kuwaruhusu wachezaji wao nane kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars ambayo leo jumatano, siku ya kalenda ya FIFA kwa mechi za kimataifa, inatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki na sudan huko jijini Khartoum. Yanga imejitetea kuwa walipata mwaliko huo kabla kabla ya wachezaji hao kuitwa timu ya taifa hivyo wana haki ya kuwatumia licha ya ukweli kwamba TFF ina haki zaidi kwani siku hii inatambuliwa na FIFA kwa kuwa ipo kwaenye kalenda ya mechi za timu za taifa na club zinawajibika kuwatoa wachezaji wote wanaoitwa. 
 Sasa Yanga kwa kitendo mlichokifanya kuwazuia wachezaji wenu wasishiriki kuichezea timu yetu ya taifa mnataka watanzania tuwaeleweje, mbona mnakosa uzalendo kiasi hiki??
Kocha wa timu ya taifa, Paulsen imebidi aokote wachezaji ambao hawakua katika list yake, sisemi kama hawana kiwango cha kutosha kuichezea timu yetu ya taifa ila kuna mambo mengi watakua wameyakosa kama kuzoeana uwanjani na mbinu ambazo wachezaji wa siku zote hufundishwa na kocha huyo, hivi timu yetu isipofanya vizuri tumlaumu Paulsen kama tulivofanya kwa Maximo au?
YANGA FC, HII NI DHARAU!!

MHIMBILI UNIVERSITY HAISAJILI TENA WANAFUNZI

Chuo cha mhimbili, MHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES (MUHAS) chafuta udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa kwanza. Inasemekana utawala wa chuo hicho hauna mpango wa kudahili wanafunzi wapya wanaotaka kujiunga chuoni hapo kwa muda wa miaka kadhaa hadi wanafunzi wote waliopo watakapomalizika.
Bado haijajulikana kama lengo la utawala ni kubadili mfumo mzima wa utoaji elimu kwa wanafunzi wapya watakaoanza tena kusoma chuoni hapo au ni kwa ajili ya marekebisho ya majengo ya chuo hicho ambayo kwa kweli hayana mvuto hata kidogo.
Skulliz blog bado inaendelea kufanya uchunguzi ili kupata habari kamili then kama kawa mzigo utadondoshwa hapa hapa live bila chenga, stay tunned brothers n sisterz

Wednesday, August 3, 2011

DIAMOND NA WEMA, Mahaba motomoto, mhm!

kumbe kweli lisemwalo huwa lipo, zilianza tetesi tetesi tu na wenyewe wakakana sana, ooh sisi ni marafiki tu, tupo karibu coz kuna kazi tunafanya pamoja, kumbe kulikua na somethig behind, its good now mmeamua kuweka wazi tu,

diamond na Wema wamechil kimahaaabaaaa





ayayayayayaaaa, jiachieni vijana, Diamond congrats sana naona mtot mzuri kabwaga zake zote kwako,

SERENGETI FIESTA 2011, Aina Majotrooooo

msanii wa kizazi kipya Prof Jay akiwarusha mashabiki ndani ya uwanja wa CCM Kirumba Mwanza

SHAGGY, Msanii wa kimataifa kutoka Jamaica akiwaburudisha mashabiki ndani ya Rock city


mashabiki wakigambeka kitu cha serengeti pale kati, full shangwe


jukwaa la fiesta 2011, ebwanaeee ni noumaa, watu kibaaoooo

Adam Mchomvu, mtangazaji Cloudz fm ndie aliekua MC fiesta ya Mza akiwazingua mashabik kama kawa

msanii Diamond akifanya bonge moja la show, salute kijana

Godzilla, tupe mambo bro.

Ludacris, msanii wa kimataifa from USA akidondosha bonge la show ndani ya viwanja vya leaders, Ludacris ndie aliekua mgeni rasmi fiesta2011, jamaa ni mkali

msanii wa kizazi kipya mwana FA au Binamu akitema rymes, kiufupi fiesta ya mwaka huu ilikua Off da hook, kama hukuweza kuhudhuria trust me, umemic bonge moja la moment