contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, November 24, 2011

MIGOMO SIO ISHU

Kwa mtazamo wangu kiukweli mimi sioni faida ya migomo no matter tunapigania kitu gani, hii ni kutokana na mambo yaliotokea hapa juzikati, baaadhi ya wanafunzi wameumizwa kwa kupigwa na askari, wengine tumeumizwa na mabomu ya machozi, hii sio mara ya kwanza kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam kugoma na kuandamana, kama kweli migomo ingekua inasaidia, haya matatizo yasingekua yanajirudia, tutaendelea kupigwa mabomu ya machozi na mwisho wa siku tutakuja kupigwa hata na risasi za moto na matatizo yataendelea kujirudia kama kawa, me nashauri tungejaribu kutafuta njia nyingine ya kuwafanya hawa viumbe watuelewe, kuna wanafunzi wa mwaka wa kwanza pia wameandamana, nyie hamjafikisha hata semista moja hapa chuo mmeshaanza kujiingiza matatizoni, mkiumizwa au kufukuzwa chuo mtawaelezea habari gani wazazi wenu ambao wanajinyima ili nyie mpate elimu, acheni kufata mkumbo wadogo zangu, someni, hicho ndicho kilichowaleta UDSM.

No comments:

Post a Comment