contact


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, November 4, 2011

CHUO CHA MAENDELEO NA USIMAMIZI WA MAJI (WDMI)

          Jina chuo cha maendeleo na usimamizi wa maji linaweza kuwa geni masikioni mwa watu, lakini chuo hichi ni moja kati ya vyuo vikongwe hapa nchini, kilianzishwa mwaka 1974 kikijulikana kama RWEGALULILA WATER RESOURCE INSTITUTE, dhumuni kubwa ikiwa ni wataalam katika fani mbalimbali zinazohusu MAJI.
         Kubadilika kwa jina na kuwa WATER DEVELOPMENT AND MANADEMENT INSTITUTE, ilifanyika mwaka 2008, baada ya chuo kupewa hadhi ya kuwa wakala wa serikali yaani Agency, mpaka sasa chuo kinatoa kozi tano katika ngazi ya Diploma, WATER SUPPLY AND SANITATION ENGINEERING, HYDOGEOLOGY AND WATER WELL DRILLING. HYDROLOGY AND METROLOGY, WATER LABORATORY TECHNOLOGY na IRRIGATION ENGINEERING. Mipango ya degree kuanza imekamilika na muda wowote WATER RESOURCE AND IRRIGATION ENGINEERING  itaanza, sasa kazi kwenu nyie wenye hamu ya kufanya kazi kwenye sekta ya maji, mnakaribishwa sana.

No comments:

Post a Comment